ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 24, 2018

UTEUZI ALIOUFANYA JPM SAA CHACHE ZILIZOPITA.

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa  mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi  ya chai Tanzania (TBT) na Mkurugenzi  wa Taasisi ya Utafiti wa kilimo Tanzania (TARI).

Katika taarifa ilitolewa na Ofisi ya Kurugenzi Mawasiliano Ikulu leo Mei 23, 2018 imeeleza kuwa Mhandisi Steven Daudi Mlote, ameteuliwa kuwa mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya chai Tanzania (TBT) na kuongeza kuwa Mhandisi Mlote anachukua nafasi iliyoachwa wazi na mtangulizi wake Mh. Anne Makinda ambae amemaliza muda wake.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo imeongeza kwamba uteuzi wa Mhandisi Mlote ulianza Mei 21, 2018.

Sambamba na hayo Rais Dkt John Magufuli amemteua Dkt. Geofrey Mkamilo kuwa Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa kilimo Tanzania (TARI),  uteuzi wake umeanza Mei 22, 2018 na anachukua nafasi ya Dkt. Fidelis Angelo Myaka ambaye amestaafu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.