ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 25, 2018

VIDEO:- SALAH AIONGOZA LIVERPOOL KUKANYAGA MGUU MMOJA KUTINGA FAINALI HUKU ROMA IKISUBIRI MUUJIZA MWINGINE.

Mo Salah ametengeneza moja kati ya muda muhimu wa thamani katika maisha yake ya soka na kwa klabu yake ya Liverpool kwa kuisogeza hatua kadhaa timu yake kuzifikia Fainali za michuano mikubwa Barani Ulaya.
Lakini yaweza kuwa sivyo kama inavyotabiriwa, kwani katika mchezo wa marudiano yaweza ukawa mgumu tofauti na inavyodhaniwa baada ya Roma kurejea mchezoni kwenye dakika za lala salama.
Waitaliano hao wamepata magoli ya jioni ya kustukiza kiasi cha kuweka akiba ya ndoto yao kama watatumia vyema mchezo wa marudiano nyumbani kwao.

Edwin Dzeko na Diego Peroti ndiyo waliwapa Roma Matumaini pengine ya kuweza kupindua matukeo katika mechi ya marudiano itakayofanyika jijini Roma Italia kila mmoja akisaidia kufunga bao moja na kufanya mchezo huo kumalika Kwa ushindi wa bao 5-2 walioupata Liverpool.

Edwin Dzeko ni dume la kuogopeka baada ya kuiongoza timu yake kuchomoza na ushindi kwa kuiaibisha Barsa bao 3-0 kwenye mchezo uliopita na hatimaye kufika hapa walipo sasa ndiye anayebaki kuwa tegemeo na hatma ya Roma. 
If Roma's fight-back took the gloss over what was until the last 10 minutes one of Liverpool finest-ever European nights, then it should not detract from Salah's masterpiece.
Hadi mwisho wa mchezo:-

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.