ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, February 15, 2018

CONTE ARUSHIWA JEZI YA MAN UNITED KWENYE MKUTANO NA WANAHABARI.



 Kupitia mkutano wake na waandishi wa habari mapema hii leo siku ya Alhamisi meneja wa Chelsea, Antonio Conte amekabidhiwa jezi ya Manchester United na Pranksters iliyosainiwa na kocha wa Man United, Jose Mourinho.

Watangazaji wa kipindi cha Italia 1 satirical show Le Iene , Alessandro Onnis na Stefano Corti walifanikiwa kukamilisha zoezi hilo baada ya jezi hiyo kusainiwa na Mourinho mwezi uliyopita huko The Lowry Hotel Manchester.

Mjumbe aliyefikisha jezi hiyo alimuonyesha Conte pia kipande cha video kutoka kwa Onnis na Corti kinachoelezea.

“Antonioooo, tume kutumia mjumbe kukuwakilishia jezi iliyosainiwa na rafiki yako mpya Joseee Mourinhoooo. Ametuambia kuwa anakupenda tazama alichokiandika hapo mbele ya jezi na kutupatia tukupe, rafiki yako , Jos amesema.” Ujumbe wa video kutoka kwa Onnis na Corti.

“Unaweza kutuahidi kuwa mchezo ujao utakao cheza dhidi yake mtakubaliana kuwa marafiki?,  tuambie, Antonio urafiki wenu utadumu milele.”

Hata hivyo Conte ameonekana kusuasua kutoa majibu na kupokea jezi hiyo wakati wa mkutano huo mbele ya waandishi wa habari na kumtaka prankster kusubiri mpaka kumalizika kwa kikao hicho.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.