ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, December 13, 2017

AGGREY&CLIFFORD YATOA MSAADA KWA KITUO CHA WATOTO WANAOISHI MAZINGIRA MAGUMU, DAR

 Meneja Uhusiano wa kampuni ya Aggrey Clifford, Martha Majura (kulia) akimkabidhi mkurugenzi wa kituo cha Sadeline Health Care Trust, Sara Kitanda (kushoto) mfano wa hundi ili kusaidia watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu. Wanaoshuhudia kutoka wa pili kushoto ni wakurugenzi watendaji wa Aggrey  Clifford, Luke Smit, Tel Akuku na Ryan Goslin.
 Wafanyakazi wa Aggrey Clifford wakigawa zawadi na kufurahi na watoto hao.
 Baadhi ya watoto wakiwa na furaha baada ya kupatiwa zawadi na kuonyeshwa faraja na upendo.
Wafanyakazi wa Aggrey Clifford katika picha ya pamoja na watoto hao wanaolelewa katika kituo cha Sadeline. --- Kampuni ya Aggrey&Clifford imetoa msaada wa fedha kusaidia kununua mahitaji kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha Sadeline Health Care Trust kilichopo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam. Mbali na msaada wa fedha, imetoa vifaa vya shule na vyakula ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kusherehekea sikukuu ya Krismasi ambapo pia wafanyakazi wa kampuni walijitolea muda wao kucheza na kufurahi pamoja na watoto hao kwa ajili ya kuwapatia faraja.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.