ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, November 14, 2017

TAKUKURU YATANGAZA DAU LA MILIONI 10 KWA ATAKAYEFANIKISHA KUNASWA KWA FISADI ALIYE TOROKA.

TAKUKURU wanamtafuta Godfrey John Gugai kwa kuwa na maisha na mali yanayozidi kipato chake bila maelezo
Huyu alikuwa mtumishi wa umma TAKAKURU na ameweza kujiptia mali nyingi, mwazoni TAKUKURU walimwita na kumhoji lakini baadae alipoona anakosa maelezo alikuwa anawapiga chenga na kukimbia nchi kupitia njia zisizo rasmi
Mpaka sasa anatafutwa bado hajaapatikana na wametangaza kwa mwananchi yoyote atakayempata atoe taarifa

TAKUKURU watatoa zawadi ya milioni 10 kwa ambaye atafanikiwa kupatikana kwa bwana huyo

Ametaja mali anazomiliki mtu huyo ikiwa ni pamoja na jengo la ghorofa nne lililopo Ununio Kinondoni, Jengo la Kifahari la ghorofa tatu

Ana nyumba za kupangisha Kinondoni, jengo la kifahari lililopo Majita Musoma, Jengo la Kifahari Kiseke Mwanza, Jengo la Kifahari Nyegezi Mwanza

Pia anailiki viwanja maeneo ya Bunju Kinondoni, Kigamboni, Buyuni Temeke, viwanja viwili Kaole Bagamoyo, Kibaha, Kihonda Morogoro, Kiyeheya Morogoro, Lukuvi Morogoro, Kisasa Dodoma, Itege Dodoma, Chidati Ngolo Mwanza, Mgongolo Mwanza, Nyamagana Mwanza, Nyamagana Mwanza, Magarika Mwanza, Makoko Musoma, Gomba Arusha, viwanja 3 Mwambani Tanga, Viwanja 2 Mwakidila tanga, gari aina ya Mitsubishi Canter, Toyota Rav 4,na pikipiki ,

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.