ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, October 23, 2017

YANGA YAKANUSHA TAARIFA YA KUWEKA KAMBI MORO.


Pamoja na taarifa kama Yanga itaweka kambi mjini Morogoro umeonyesha kuendelea kufanya siri jambo hilo.

Taarifa za Yanga kuweka kambi mjini Morogoro kujiwinda dhidi ya Simba Agosti 28 zilianza juzi lakini uongozi wa Yanga kutotaka kuliweka hadharani jambo hilo.

Msemaji wa Yanga, Dismas Ten amesisitiza kwamba watatangaza kambi yao ilipo baada ya kufika Dar es Salaam.

“Kwa sasa tuko Shinyanga, tutakapofika Dar es Salaam tutatangaza kambi yetu ni wapi, si sasa,” alisema.

Taarifa nyingine zinaeleza, Kocha George Lwandamina alivutiwa na kambi ya Morogoro ambayo aliitumia kujiandaa wakati wa Pre Season.

“Kocha aliipenda sana kambi ya Morogoro, utulivu na hali ilivyo. Nina uhakika kocha atataka Morogoro,” kilieleza chanzo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.