ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, September 20, 2017

VIJANA DAR WAANZA MASOMO YA TEHAMA.

Sehemu  ya  Darasa  la  Vijana  wa  Shule za  Msingi kutoka  sehemu  mbalimbali.
 Meneja  Mradi  wa Aitel  & DTBI Computer Lab, Agape  Jengela  akizungumzia  kuhusu  mradi  huo  wa  Airtel  Fursa ambao  umenza  na  Darasa  la Vijana  wa Shule  za  Msingi  kutoka  sehemu  mbalimbali  za  jiji  la  Dar  es  Salaam, katika  fursa  hiyo  Watoto wamejifunza  kutengeneza  ROBBOT.
 Sehemu  ya  Darasa  la  Vijana  wa  Shule za  Msingi kutoka  sehemu  mbalimbali.
 Sehemu  ya  Darasa  la  Vijana  wa  Shule za  Msingi kutoka  sehemu  mbalimbali.
 Sehemu  ya  Darasa  la  Vijana  wa  Shule za  Msingi kutoka  sehemu  mbalimbali.
Sehemu  ya  Darasa  la  Vijana  wa  Shule za  Msingi kutoka  sehemu  mbalimbali.
 
Vijana Dar waanza Masomo ya Tehama
Kampuni yasimu za mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na Atamizi ya Teknohama ya Dar es Salaam (DTBi)  imeanza kutoa mafunzo ya Tehama kesho katika maabara ya kompyuta iliyopo katika shule ya msingi kijitonyama na kuwawezesha vijana zaidi ya 20 waliojiandikisha kuanza kupata mafunzo hayo.

Mafunzo hayo yameanza kufatia Airtel na DTBi kutangaza kuanza kwa mafunzo hayo na kuwaalika vijana kuanzia ngazi ya shule za msingi,sekondari, vyuo vikuu na wafanya biashara kujiandikisha na kufaidika na mafunzo haya yatakayowasaidia kuvumbua application mbalimbali, kuwapatia vijana ujuzi katika mswala ya Tehama na pia kuwawezesha vijana wajasiriamali kuendesha shughuli zao za kibiashara kwa kutumia technologia za kisasa

Akiongea kuhusu kuanza kwa mafunzo hayo, Meneja Mradi wa Airtel Bi Jane Matinde alisema, Tumefurahishwa sana na muitikio mkubwa uliofanya na vijana hususani wa shule hii ya msingi ya kijitonyama na watoto kutoka maeneo mengine katika kujiandikisha na kuanza mafunzo haya. Tayari tunao jumla ya wanafunzi 20 ambapo wamejipanga kuanza kujifunza kesho kuanzia saa 9 mchana hadi saa 11 jioni.  Tunaamini hii ni fursa muhimu sana kwa vijana wetu wenye kuonyesha  dhamira yao ya kubobea katika maswala ya Tehama na komputa ya sayansi kuanza sasa wakiwa katika umri mdogo.

Bado tunapokea maombi ya kujiunga hivyo tunatoa wito kwa vijana wa sekondari , wale waliomaliza darasa la saba , wafanyabiashara kutumia vyema maabara hii yenye lengo la kuwezesha jamii  hususani vijana kuongeza ujuzi na ueledi kwenye maswala ya technologia na Tehama kwa ujumla.

Kwa upande wake Meneja wa maabara ya Airtel Fursa , Agape Jengela alisema “ Tayari tumejipanga kutoa mafunzo kwa vijana, walimu wamejipanga vyema katika kuhaikisha vijana hawa wanapata mafunzo bora. Mafunzo hayo ni pamoja na lego Robotics, program za uhuishaji kwa watoto(ziitwazo scratch) na ubunifu na uchapishaji wa“3D objects”  msingi wa kompyuta, uelewa wa kompyuta, kutengeneza program mbali mbali

Bado tunapokea maombi,   Tunato wito kwa wazazi na walezi kuwaandikisha vijana wao kwa kupitia  www.teknohama.or.tz na  www. airtelfursa.com  au kwa kutembelea maabara  iliyopo katika shule ya msingi kijitonyama

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.