ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 19, 2017

TAARIFA YA AJALI YA TRENI NA DALADALA YA KUTOKA GONGO LA MBOTO Alfajri leo Aprili 19, 2017.

Mtu mmoja amefariki dunia baada ya kutokea ajali ya basi la abiria/daladala (T 435 DGG) kutoka Gongo la Mboto kwenda Mnazi Mmoja kuigonga treni ya Pugu leo Aprili 19, 2017 saa 11 alfajiri katika makutano ya reli na barabara ya Nkurumah jijini Dar es Salaam.

Majeruhi wa ajali ni 23 , wanane wapo hospitali ya Amana na waliobakia 15 wapo Hospitali ya Taifa Muhimbili MOI watatu kati yao ni mahututi. Taarifa zaidi itatolewa kuhusu ajali hiyo.

Hata hivyo treni ya Pugu inaendelea na huduma zake kwa kufuata ratiba.

Imetolewa na Afisi ya Uhusiano kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TRL

Nd. Focus Sahani,
Dar es Salaam,
Aprili 19, 2017.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.