ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 21, 2017

KANDA YA ZIWA SASA KUMULIKWA USIKU NA MCHANA NA 'SUN KING' SANJARI NA KUWA NA MAZINGIRA SALAMA.

Afisa Tawala wilayani Nyamagana, Zubeda Kimaro (mbele), akizindua ofisi ya Sun King Jijini Mwanza ikiwa ni uzinduzi rasmi wa kampuni hiyo kitaifa hii leo. Kulia ni Mkuu wa Masoko wa kampuni ya Sun King Tanzania, Judie Wu.
Meneja Masoko wa kampuni ya Sun King nchini Tanzania, Albert Msengezi, akizungumza na wanahabari kwenye uzinduzi rasmi wa ofisi na bidhaa za Sun King nchini, uliofanyika hii leo Buzuruga Plaza Jijini Mwanza.
Mgeni Rasmi, Afisa Tawala wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, Zubeda Kimaro, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, kwenye uzinduzi rasmi wa ofisi na bidhaa za Sun King nchini Tanzania, uliofanyika Buzuruga Plaza Jijini Mwanza hii leo.
Mkuu wa Masoko wa kampuni ya Sun King Tanzania, Judie Wu, akizungumza na wandishi wa habari kwa maswali ya ufafanuzi kupitia kusanyiko la uzinduzi rasmi wa ofisi na bidhaa za Sun King nchini Tanzania, uliofanyika Buzuruga Plaza Jijini Mwanza hii leo.
Wadau mbalimbali katika kusanyiko la uzinduzi rasmi wa ofisi na bidhaa za Sun King nchini Tanzania, uliofanyika Buzuruga Plaza Jijini Mwanza hii leo.
Mstari wa mbele kusanyiko la uzinduzi rasmi wa ofisi na bidhaa za Sun King nchini Tanzania, uliofanyika Buzuruga Plaza Jijini Mwanza hii leo.
Kwa umakini kuzingatia yaliyomo.
Sun King.
Kwa umakiini zaidi.
Kusanyikoni.
Mbele ya mjengo uliopo Buzuruga Plaza Mwanza.
Meneja Masoko wa kampuni ya Sun King nchini Tanzania, Albert Msengezi,akifunguka juu ya faida na matumizi ya taa za sola.
Afisa Tawala wilayani Nyamagana, Zubeda Kimaro (mwenye kofia) akipokea maelezo kuhusu faida na uimara wa baadhi ya taa za Sun King kupitia jumba la ofisi ya Sun King Jijini Mwanza ikiwa ni uzinduzi rasmi wa kampuni hiyo kitaifa hii leo, kushoto mtoa maelezo ni Mkuu wa Masoko wa kampuni ya Sun King Tanzania, Judie Wu.


















Wakazi wa maeneo ambayo bado hayajafikiwa na huduma ya umeme nchini, wanatarajiwa kunufaika na huduma hiyo kupitia mitambo ya umeme wa jua kwa bei nafuu inayosambazwa na kampuni ya Sun King.



Meneja Masoko wa kampuni hiyo nchini, Albert Msengezi, ameyabainisha hayo hii leo Jijini Mwanza kwenye uzinduzi rasmi kitaifa wa bidhaa za Sun King ambazo ni taa za sola pamoja na majiko bunifu ya Jikokoa.



“Kila Kijiji nchini tunakusudia kuwa na mawakala wa kampuni ya Sun King ambao watawafikia wananchi wote wanaoishi katika maeneo hayo na hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu tunakusudia kuwa na wanufaika zaidi ya Milioni Moja ambapo tumejikita kwenye bidhaa bora zisizochafua mazingira ikiwemo taa za sola na majiko yasiyochafua mazingira”. Amebainisha Msengezi.



Mkuu wa Masoko wa kampuni ya Sun King, Judie Wu, amesema kampuni hiyo imedhamiria kuhakikisha kila mmoja Mjini na Vijijini anapata huduma ya umeme pamoja na kutumia majiko bunifu yasiyo na madhara kiafiya kwa bei nafuu.


Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwenye uzinduzi huo wa bidhaa za King Sung, Zubeda Kimaro ambaye ni Afisa Tawala wilayani Nyamagana, amewahimiza wawekezaji kujitokeza kwa wingi kuwekeza mkoani Mwanza kwani kuna fursa nyingi za kiuwekezaji hatua ambayo pia itazalisha ajira zaidi kwa vijana.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.