ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 25, 2016

NAIBU WAZIRI WA AFYA DK. KIGWANGALLA AKAGUA MAABARA YA HOSPITALI YA KISHAPU


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi  Kigwangalla amezitaka Maabara Nchini kuhakikisha zinafuata misingi na kanuni sahihi katika kuzingatia ubora  na ufanyaji.

Akiwa katika ziara ya kikazi katika Mkoa wa Shinyanga, Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla aliweza kukagua Maabara ya Hospitali ya Wilaya ya Kishapu  ambapo alibaini mambo mbalimbali yakifanywa bila kuzingatia taratibu sahihi za Mabara huku akiagiza Mganga Mkuu wa Wilaya kuhakikisha wanarekebisha mapungufu hayo katika Maabara hiyo.

Miongoni mwa mambo ambayo alikuta katika Maabara hiyo ni pamoja na kutokuwa na taratibu za kiutendaji hasa kwa wafanyakazi wenyewe wa Maabara ambao walishindwa kuzingatia vigezo na msharti ambayo taratibu za Maabara zinahitaji.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi  Kigwangalla akikagua Maabara hiyo ya Hospitali ya Wilaya ya Kishapu.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi  Kigwangalla akiangalia moja ya mashine ndani ya Maabara hiyo ambayo wataalamu wa Maabara hiyo hawajaweza kuweka viambata vya kuonyesha kama imefanyiwa matengenezo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi  Kigwangalla akitoa maagizo namna ya Maabara inavyotakiwa iwe na taratibu zake.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi  Kigwangalla akiagana na wafanyakazi wa Hospitali hiyo ya Kishapu
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi  Kigwangalla akiagana na wafanyakazi wa Hospitali hiyo ya Kishapu

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.