ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 1, 2013

LOWASSA AZINDUA VIKOBA KWA AKINA MAMA MWANZA

Waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa (wapili kutoka kulia) akikata utepe wa kuashiria uzinduzi wa Vikoba vya umoja wa wanawake wa madhehebu ya Kikristo Mwanza, kulia ni askofu wa Kanisa la Anglican Diosisi ya Nyanza (DVN) Boniface Kwangu akiwa ameshikilia kiasi cha shilingi millioni 40 zilizochangwa ikiwa ni pamoja na hudhi na ahadi zilizowekwa kutunisha Vikoba, Mkuu wa mkoa wa Simiyu Paschal Mabiti pia anaonekana pichani wa pili kushoto .
Na Albert  Sengo.
WAZIRI Mkuu Mstaafu Edward Lowassa amewapongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Rais wa Serikali ya Zanzibar Dkt.Mohamed Sheni kwa njisi ambavyo wamekuwa wakikazia suala la kudumisha amani nchini, wakiwemo viongozi wa Taasisi za kidini Kalidinali, Askofu Mkuu Polycarp Pengo (Romani),Askofu Alex Malasusa (KKKT), Mufti Shekhe Mkuu wa Tanzania  Simba Bin Simba na viongozi wengine wakiwemo wachungaji wa madhehebu mbalimbali nchini.

Lowassa alitoa pongezi hizo leo wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa Vikoba vya umoja wa wanawake wa Madhehebu ya Kikristo Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela uliofanyika katika Kanisa la D.V.N Angilikana lililopo Nyamanoro Wilayani Ilemela  na kueleza kwamba viongozi hao wamekuwa wakikemea udini na kutaka watanzania kuendelea kuilinda amani ya nchini kama mboni ya jicho kwani kuipoteza Amani tuliyonayo nchini itatugharimu maisha kuirejesha hivyo amewasihi watanzania wasichoke na Amani ambayo ni kama hewa ikitoweka haiwezi kurudi tena kamwe.
Lowassa amewataka watanzania wote kuwasikiliza viongozi hao na kuwaunga mkono katika kukemea watu wanaotaka kuwatumia na kusababisha vurugu ili amani tuliyonayo nchini iweze kupotea kwa masilahi yao. 
Sikiliza alichosema.... 



Maandamano yalifanyika kutoka viwanja vya furahisha hadi Kanisa la D.V.N Angilikana lililopo Nyamanoro Wilayani Ilemela kwaajili ya uzinduzi wa Vikoba vya umoja wa wanawake wa Madhehebu ya Kikristo Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela. 
Hatimaye maandamano yalifika katika Kanisa la D.V.N Angilikana lililopo Nyamanoro Wilayani Ilemela.


Ilikuwa ni majira ya saa 3:45 asubuhi na hii ni sehemu ya kusanyiko lililofika kanisani hapa  kwaajili ya kushuhudia uzinduzi wa Vikoba vya umoja wa wanawake wa Madhehebu ya Kikristo Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela.


Kwaya ya Anglican Nyamanoro Mwanza nayo ilihudumu kwenye ya uzinduzi wa Vikoba vya umoja wa wanawake wa Madhehebu ya Kikristo Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela.


Watu wa mataifa mbalimbali nao wamekuja katika kusanyiko hili Kanisa la D.V.N Angilikana lililopo Nyamanoro Wilayani Ilemela kwaajili ya uzinduzi wa Vikoba vya umoja wa wanawake wa Madhehebu ya Kikristo Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela.


Sambamba na tukio la uzinduzi wa vikoba lililofanyika kanisani hapa vilevile ikumbukwe kuwa siku hii ni sehemu ya Maadhimisho ya Maombezi ya kinamama duniani hivyo akinamama walifanya maombezi hayo kisha baadaye ukafuata uzinduzi uliosimamiwa vyema na mh. Lowassa.


Ibada ya maombezi ikiendelea kanisani.


Umoja wa akinamama wa Madhehebu ya Kikristo Mwanza ukimkabidhi zawadi Mh. Lowassa kwaajili ya mkewe ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Maombezi ya Kinamama Duniani katika Kanisa la D.V.N Angilikana lililopo Nyamanoro Wilayani Ilemela. 


Umoja wa akinamama wa Madhehebu ya Kikristo Mwanza pia ulimkabidhi zawadi ya Biblia Mh. Lowassa ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Maombezi ya Kinamama Duniani katika Kanisa la D.V.N Angilikana lililopo Nyamanoro Wilayani Ilemela. 


Umoja wa akinamama wa Madhehebu ya Kikristo Mwanza pia ulimkabidhi zawadi ya Biblia Mh. Lowassa ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Maombezi ya Kinamama Duniani katika Kanisa la D.V.N Angilikana lililopo Nyamanoro Wilayani Ilemela.


Aidha Mbunge huyo wa Jimbo la Monduli na Mjumbe wa NEC CCM Taifa wa Wilaya ya Monduli amewataka wanasiasa wote nchini kumuunga mkono kuiomba serikali kurudisha fedha za Mabilioni ya JK na kuhakikisha yanapelekwa moja kwa moja kwa wanawake wa vijijini walioanzisha VICOBA ili kuwasaidia kujikwamua kiuchumi hali ambayo itawawezesha wanawake wengi kuondokana na umasikini. 

Sikiliza alichosema..

Utaifa zaidi ndani ya kwaya ya kanisa la DVN.

Aidha amewataka watanzania wote kuwasikiliza viongozi hao na kuwaunga mkono katika kukemea watu wanaotaka kuwatuawa  na kusababisha vurugu ili amani tuliyonayo nchini iweze kupotea kwa masilahi yao kamwe wasikubali hivyo ni vyema wakaungana kuwakataa kwa nguvu zote kwani hadi sasa wagombea Urais wan chi ya Kenya wanawataka wakenya kuwa kama watanzania hivyo hivyo na Waganda wamekuwa wakihubiliwa kutuiga kutokana na umoja na amani tuliyonayo hapa nchini.


Furaha ya mchungaji na mwanae.


Katika kuuzindua mfuko wa Vikoba vya umoja wa wanawake wa Madhehebu ya Kikristo Jiji la Mwanza, Mfanyabiasha ambaye ni mkurugenzi wa Gold Crest Hotel, Bw. Mathias Manga alitoa cheki yenye thamani ya shilingi millioni 5.


Waziri mkuu mstaafu Mh. Edward Lowassa akimpa mkono wa pongezi MNEC wa Busega Bw. Raphael Chegeni mara baada ya kuwasilisha mchango wake wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa Vikoba vya umoja wa wanawake wa Madhehebu ya Kikristo Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela uliofanyika katika Kanisa la D.V.N 


Furaha. 


Saa 6:30 mchana shughuli ya uzinduzi inamalizika na Mh. Lowassa anaondoka eneo la tukio huku akipeana mkono na waumini. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.