ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, December 15, 2011

WANA MWANZA DAR MPOooooooo?

Wadau wa mwanza timu ya mpira wa kikapu mkoa wa mwanza (rocky city team) ipo katika mashindano ya Taifa cup jijini dar. Mpaka sasa timu hiyo imeshacheza mechi 2, mechi ya kwanza ilikuwa dhidi ya Zanzibar ambapo Zanzibar walishinda vikapu 56 vs Mwanza 55,game ya pili Mwanza iliigagadua Tanga kwa jumla ya vikapu 71 vs 40, Leo Mwanza imeshuka uwanjani kupepetana na timu ya mkoa wa Rukwa iwapo itashinda basi itakuwa ni tiketi kuingia hatua ya robo fainali.

Robo fainali itaendelea kesho sambamba na nusu fainali na fainali itakuwa jumamosi.
Uongozi wa basketball wa mkoa wa Mwanza unatoa wito kwa wana mwanza wote popote walipo hasa waliopo jijini Dar wajitokeze kwa wingi kuipa support timu yao ya mkoa iwe kwa hali na mali ukizingatia inakabiliwa na ukata kwani wadhamini TBL kupitia Castle lite wametoa shilingi laki 9 tu kwa kila timu hivyo gharama zingine ni juu ya mkoa wenyewe.

Hima hima mwenye maji ya kunywa ayaa, chakula ayaa, nauli ayaa na kulala pia. Timu inaishi Topland hotel Magomeni Mapipa na viwanja vya mashindano ni Don Bosco Upanga na Leaders Club.


Ni chini ya coach Robert Mwita, Timu ya mkoa wa Mwanza inaundwa na wachezaji Bundala Charles, Enock Charles, Ahmed Said, Vincent Shinda, Francis Shilinde, Wilson Sajigwa Masanja, Adam Jegame, Juma Kissoky, Mahamed Ally Dibo, Amri Mohamed, Amon Diba Semberya, Chacha Mukolo Tubert na Kizito Sosho Bahati.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.