ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, June 14, 2011

SPRITE STREEET BASKETBALL BONANZA MWANZA

Juzi J2 watu walifunga mtaa wa Bantu Mwanza na kukusanyika eneo la mbele la kiunga cha vinywaji, vichomwa na vitafunwa 'Salma Cone' kisha michezo ya Sprite Street Basketball Bonanza ikafanyika.

Mashindano hayo yaliyokuwa na mvuto wa kipekee yalivuta hisia za wengi kwani yalihusisha vijana wenye ujuzi wa kutupia kikapu toka pande na pande za Rock city kama vile vyuo, mashule na kitaani.

Hupiti mzazi...!!

Most valuable Player (MVP) Hemedi akipokea zawadi zake toka kwa msimamizi wa mashindano hayo Mwanza, Mr. Rutta wa Nyanza Bottling Co. Ltd.

Washindi wa kwanza timu za basket wachezaji wa4-wa4 walijishindia mipira mitatu, t-shirt na kofia.

Washindi wa tatu timu za wachezaji wa4-wa4 na zawadi zao T-shirt na Kofia toka Spite.

Pia kulikuwa na mashindano ya mitupo kwa washiriki wa kawaida ambao hawajawahi kuucheza mchezo wa Basket kama pichani inavyoonekana wakiwa kwenye mstari zamu kwa zamu.

Washindi walipatikana na kuzawadiwa, dekshia mjunki smile lake.

Mashabiki na wacheza katika engo moko.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.