ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, January 17, 2011

HAPA NA KULEee!...! ' KOSHA MACHO NDUGU'

Wanauzwa hawa! Maubunifu katika utafutaji ngawira.

Ukitaka swala, twiga, bata we mwenyewe tu! Ni kunakshi tu bustani na wanyama Feki.

Wabongo bwana OOOh oh pesa za sasa hivi hamna kitu' laini kama karatasi za kunyongea..., zinachafuka upesiii, ukiishika kwenye kiganja muda mrefu inapoteza uboraaaa.. Ziko kama feki feki hiviii..(Nimeshuhudia mwenyewe kwa baadhi ya watoa huduma hususani daladala wakizikataa fedha hizo). Je! wewe unazionaje, Je! Umezipendaaa?

Mzalendo akidadisi vihusishi vya noti mpya kutoka katika matangazo ya noti zetu mpya kwenye kuta za mitaa ya kituo cha stendi ya sahara.

Watoto hawa wa mitaani wanaonekana kila siku eneo hili lililo katikati ya jiji pembezoni mwa uzio wa benki moja, wakiombaomba kisha kucheza kamali baina ya wao kwa wao. Tunawatizama tu! biashara inaendelea..

Wajameni uchafu ni mazoea ama mauzembe?

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.